Thursday, July 3, 2014

Fuatilia mapumziko ya LADY JIDE (@JideJaydee) akiwa USA kupitia website yake hii mpya

Nimeanza safari za hapa na pale, kutulia ni mpaka mwezi August. Unaweza kusafiri na mimi kwa picha kupitia www.jidejaydee.com au kupitia Diary ya Lady JayDee ‪#‎EATV‬ ‪#‎Sundays‬ ‪#‎9pm‬.
Karibuni kwenye ulimwengu wangu.

Huyu hapa Mchezaji mwingine wa Yanga aliyehamia Azam Fc.

Taarifa ambayo imekua kama ya ghafla ni kuhusu Aliyekuwa mchezaji kiungo wa Yanga Athumani Iddi ‘Chuji’ kijiunga na timu ya Azam Fc na asubuhi ya leo ameonekana akiwa mzoezini Uwanja wa Azam Complex Chamazi, Dar es Salaam.



Wednesday, March 12, 2014

TUNDAMAN AMBADILI MASOGANGE

KIBAO cha Msambinungwa cha mkali wa Bongo Fleva, Khalid Ramadhan ‘Tundaman’ kimegeuka mwiba kwa Video Queen, Agnes Gerald ‘Masogange’ ambaye ameuza sura kupitia video ya wimbo huo, kwa sababu watu mitaani wameacha jina lake halisi na kumwita Msambinungwa.

Khalid Ramadhan ‘Tundaman’. Akisebeza na Stori Mix, Tundaman alisema, maana ya jina la kibao chake hicho ni mwanamke ambaye hajatulia – mapepe na ameshaelezea maana hiyo kwenye vyombo mbalimbali vya habari, ndiyo maana Masogange anachukizwa anapobadilishwa jina na kupewa hilo.
“Masogange ameshanipigia simu mara nyingi  akinilalamikia kuitwa hilo jina. Sikuwa na nia mbaya na wala sikumlenga yeye.
Ajue kuwa pale alivaa uhusika usio wake, si kweli kuwa tabia zilizoelezwa kwenye kibao hicho ni zake. Watu waache kumuita hilo jina na yeye pia aachane na maneno ya watu.”

WEMA SEPETU ALIA KUTOPATA MTOTO!

MASKINI! Kilio kikubwa cha Wema Isaac Sepetu ni kupata mtoto, Risasi Mchanganyiko linafunguka.
Habari zilieleza kuwa Wema amekuwa na kiu ya mtoto kwa muda mrefu na kwamba alishakuwa na wanaume tofauti lakini hawakumpatia mtoto.


Ilisemekana kwamba katika msururu wa wanaume aliominya nao kimalavu, iliwahi kuripotiwa kuwa ni mwanaume mmoja tu aliyefanikiwa kumpa ujauzito lakini kwa bahati mbaya mimba ilichoropoka.
Mwanaume aliyekuwa na mzigo huo ilidaiwa ni Prezidaa wa Bendi ya Mashujaa Musica, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’.
Baada ya kupania kwa muda mrefu bila mafanikio, ilidaiwa kuwa mwanadada huyo mkali wa sinema za Kibongo aligeuzia mapenzi yake kwa mbwa (pets) wake wawili, Van na Gucc ambao mmoja wao amezaa hivi karibuni.
Habari zinadai kuwa, kutokana na mapenzi yake na mbwa hao, amekuwa akiwagharamia mkwanja mrefu katika chakula na shopping za mavazi ya bei mbaya. WEMA ANAFAFANUA
“Nawapenda sana mbwa wangu, nawaona kama ndiyo watoto wangu kwani sina mtoto na ninatamani sana ila najua Mungu atanijalia siku moja muda ukifika,” alisema Wema na kuongeza:
“Kila jambo na wakati wake, nitapata tu, nadhani ni suala la muda tu. Watu wanaweza kushangaa namna ninavyowapenda mbwa wangu, nawathamini kwa sababu wananipa faraja na nipo nao karibu. Nawajali kama binadamu.”
Kabla ya Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ anayetoka naye kwa sasa, wengine waliowahi kuonja penzi lake na wakashindwa kumpatia mtoto ni pamoja na marehemu Steven Kanumba, Jumbe Yusuf na Chaz Baba.

MAHAKAMA YAWARUHUSU BASIL MRAMBA NA DANIEL YONA KWENDA KUTIBIWA NJE

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imewaruhusu kwenda kutibiwa nje ya nchi  Mawaziri Waandamizi wa zamani,  Basil Mramba na Daniel Yona wanaokabiliwa na tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia Serikali hasara ya Sh. bilioni 11.7  kwa kutoa msamaha wa kodi baada ya kusikiliza maombi yao leo.
 
Uamuzi huo umetolewa leo mahakamani hapo na Jaji John Utamwa baada ya washtakiwa hao kuwasilisha maombi ya kwenda kutibiwa nje ya nchi.
 
Upande wa Jamhuri ulidai kuwa hauna pingamizi na maombi hayo.
 
Jaji Utamwa alisema baada ya kusikiliza maombi hayo mahakama inawaruhusu washtakiwa kusafiri kwenda nje ya nchi kutibiwa na kwamba pamoja na ruhusa hiyo Mramba na Yona siku ya kusikiliza kesi Aprili 22, mwaka huu wahudhurie mahakamani.
 
Mbali na Mramba na Yona, mshtakiwa mwingine ni, Katibu Mkuu wa zamani wa Wizara ya Fedha, Gray Mgonja.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa Aprili 22 hadi 25, mwaka huu.
 
Katika kesi ya msingi, washtakiwa wanadaiwa kuwa, kati ya Agosti mwaka 2002 na Juni 14 mwaka 2004 jijini Dar es Salaam, wakiwa watumishi wa umma kama mawaziri na katibu mkuu walitumia vibaya madaraka.
 
Ilidaiwa kuwa kwa kupitia kampuni ya Alex Stewart (ASSAYERS) ya Uingereza iliyoingia mkataba wa ukaguzi wa madini ambapo kwa kupitia kampuni tanzu ya Alex Stewart ( ASSAYERS) Government Business Corporation  waliingia mkataba kukagua kiwango cha uzalishaji wa madini ya dhahabu kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma.

Sunday, December 8, 2013

ARSENAL YASHIKWA EPL, YALAZIMISHWA SARE YA 1-1 NA EVERTON

Mesut Ozil akiifungia Arsenal bao la kuongoza katika dakika ya 80 ya mchezo

 Ozil akishangilia na wachezaji wenzake baada ya kufunga bao.…


Gerard Deulofeu wa Everton (kushoto) akishangilia bao la kusawazisha dakika ya 81 ya mchezo.


Beki wa Arsenal Laurent Koscielny (kushoto) akijaribu kumzuia Steven Pienaar wa Everton wakati wa mchezo huo.
Timu ya Arsenal imeshikwa baada ya kutoka sare ya 1-1 na Everton katika mechi ya Ligi Kuu England iliyopigwa Uwanja wa Emirates jijini London, Uingereza hivi punde.
Bao la kuongoza la Arsenal limewekwa kimiani na Mesut Ozil dakika ya 80 kabla ya Gerard Deulofeu kusawazisha bao hilo dakika ya 84 na kufanya matokeo kuwa 1-1.
Mpaka mwisho wa mchezo Arsenal 1 na Everton 1. Kwa matokeo hayo bado Arsenal wanaongoza ligi hiyo wakiwa na pointi 35 wakati Everton wapo nafasi ya tano wakiwa na pointi 28.

Wednesday, November 13, 2013

PICHA:NDANI YA STUDIO YA DAVIDO TUKIMALIZIA AUDIO YA NUMBER 1 REMIX

 Siku zote sitoacha kumshukuru Mungu kwa kila hatua
ninayopiga katika safari yangu ya Music,na sitokutendea 
haki nisiporudisha shukrani za dhati 

kwa wewe shabiki yangu wa kweli unae 
endele kunipa sapoti inayonifanya nizdi kukaza 
kukutengenezea mambo mazuri zaidi..hii ikiwa ni ziara
 yangu mhimu kabisa nchini Naija,kwa ajili ya kupika kile
 unachkisubilia kwa hamu,my number one remix na
 mwanangu Davido,hii ilikuwa ni jana usiku
 tukiwa studio,hii ni studio ya Davido iliyopo nyumbani
kwake na kkubwa tulichokuwa tunakifanya ni kumalizia kabisa 
audio kabla ya kuingia mzigoni kushoot kideo.......
 
 
 
 Team yote hii ni kuhakikisha kila kitu 
kinaenda sawa kabisa..Babu tale kwa mbali mwenyewe kamechishaa.....!!!