Wednesday, October 3, 2012

NICK MINAJ NA MARIAH CAREY WAZINGUANA TENA......NICK ATEMA MVUA YA MATUSI




Nick Minaj

Wiki chache baada ya Mariah Carey kukanusha tetesi kuwa alikuwa na beef na Young Money Queen Nick Minaj ambae ni jaji mwenzake kwenye American Idol sasa mambo yamekuwa tofauti baada ya video yenye picha tofauti kabisa na kile kilichoelezwa na Carey kusambaa kwenye mitandao.

Video hiyo inaonesha Nick Minaj akiwa kakasirika na anampa makavu live Mariah Carey,Tukio hili limetokea wakati wanaendelea na kazi yao ya kujaji washiriki mbalimbali na safari hii walikuwa Charlotte, North Carolina. 
 
Mtu mmoja ambae alishuhudia live tukio hilo amesema kuwa Nick Minaj alionekana kupandisha mzuka na kufikia hatua ya kumtishia the R&B diva Mariah Carey na kusema “I’m gonna knock you out”.

Chanzo hicho kiliendelea kusema kuwa Nick Minaj aliongea kwa sauti ya juu sana na kumtolea matusi makali Mariah Carey akisema “I told them, I’m not f***kin’ putting her f**kin’ highness there.”  Lakini hii sehemu haikushikwa na lensi ya camera hiyo iliyokuwa inachukua matukio ya American Idol.

Inasemekana kuwa hii varangati ilitokea baada ya kutofoutiana sana katika maamuzi kwa washiriki walio-perform siku hiyo. Wakati hayo yanatokea, Nick Minaj na Mariah Carey walikuwa wamekaa kwenye meza ya majaji, na jaji mwenzao Keith akiwa amekaa katikati yao na Randy Jackson akiwa amekaa mwishoni upande wa Mariah Carey.

Kutokana na hali hiyo watayarishaji wa American Idol iliwalazimu kusimamisha performance ya siku hiyo ili majaji hawa wacool down kwanza. 
 
Hali hii inaonekana kuwatishia waandaji wa American Idol na wana wasiwasi kama Nick Minaj na Mariah Carey watadumu kwa muda mrefu wakiwa wanafanya kazi yao pamoja kama majaji wa American Idol.
 
                                                   Mariah Carey

No comments:

Post a Comment