Monday, June 18, 2012

ITALY VS IRELAND:KUMTEGEMEA SANA ANDREA PIRLO NI HATARI KWA ITALIA

Kuna suala la kubishana kidogo kwamba Andrea Pirlo alikuwa ndio kiungo bora wa ulaya msimu uliopita. Alisajiliwa na Juventus na kuisadia kushinda taji la kwanza la serie A tangu ilipotokea skendo ya Calciopoli ya mwaka 2006; chini ya Pirlo Juventus walimaliza msimu bila kufungwa kwenye ligi, na Andrea Pirlo aliifanya bibi kizee wa Turin kutisha tena.

Utulivu na uvumilivu wa Pirlo akiwa na mpira ulikuwa hauna mfano mwingine kwenye bara la ulaya, na akiwa anaelekea kwenye Euro 2012, alikuwa kwenye kiwango cha maisha yake.



MIDFIELD MAESTRO
PIRLO'S STATS VS SPAIN
PASSES MADE
LONG PASSES
SHORT PASSES
PASSING ACCURACY
GOALS
ASSISTS

39
9
30
82.1%
0
1
PIRLO'S STATS VS CROATIA
PASSES MADE
LONG PASSES
SHORT PASSES
PASSING ACCURACY
GOALS
ASSISTS

67
11
56
82.1%
1
0


Akiwa na miaka 33, kiungo mchezeshaji huyo hakutegemewa kucheza kwa kiwango kizuri kwenye msimu wa 201-12. Aliachwa na AC Milan kwa kuwa na umri mkubwa, lakini chini ya uongozi wa Antonio Conte, akaweza kuwa mhimili mkuu wa timu hasa kwenye eno la kiiungo.

Kiwango chake kikubwa kiliwafanya Italia waende kwenye michuano ya Euro nchini Poland na Ukraine wakiwa kwenye hali ya matumaini. Kama ilivyo Juve, kocha Cesare Prandelli amemfanya Pirlo ndio nguzo ya timu yake; huku akicheza pembeni ya Claudio Marchisio na Thiago Motta kwenye kiungo, ilionekana kwamba Azzuri wangepita kwenye hatua ya makundi bila wasiwasi wowote.

Baada ya mechi ya kwanza dhidi ya Spain, ambayo Italy walionekana kucheza vizuri. Walipata suluhu ya kuipigani sana ya 1-1 dhidi ya mabingwa watetezi. Azzuiri walionekana kuwa vizuri kwenye ulinzi, mawinga na ushambuliaji wa mtu kama Di Natale mwenye uwezo wa kufunga mabao muhimu, lakini kubwa kuliko ilikuwa na kiwango cha Pirlo aliyecheza dhidi ya midfield maestros Xavi na Iniesta.

"Mchezaji aliyeleta tofauti kubwa ni Pirlo," Fabio Capello aliiambia UEFA.com. "Kila mara alipoanzisha shambulizi, lilikuwa ni shambulizi la hatari kwa wapinzani Spain."

Corriere dello Sport lilisema kwenye gazeti la asubuhi ya siku iliyofuatia "Beautiful Italy". Lakini gazeti hilo halikuendeleza sifa hizo siku nne baadae, likaandika, "Sare & Shida" kama kichwa cha habari baada ya vijana wa Prandelli kutoka suluhu na Croatia katika mechi ya pili ya kundi C.

Italy walihangaika na kucheza hovyo, hasa kwenye kipindi cha pili, wakipewa presha kubwa na kikosi cha Bilic, na hatimaye wakaruhusu goli la kusawazisha kwa Croatia likifungwa na Mandzukic. Pirlo alitulizwa hasa kwenye dakika 45 za kipindi cha pili, na matokeo yake timu ya Italia ikaonekana imevunjika vipande vipande.

Imekuwa hali kma inayoitokea Portugal kumtgemea sana Ronaldo, Pirlo asipokuwa kwenye kiwango kizuri basi na Italia inapotea kabisa.

Akiwa ndio tishio pekee kwenye creative department, Pirlo alikuwa ndio target kwa vijana wa Slaven Bilic. Alikabwa vilivyo na viungo wa Croatia chini Ognjen Vukojevic,  na hivyo kupelekea kushindwa kucheza vizuri.

Suluhisho pekee kwa Prandelli, ni kuongeza kiungo mwingine mbunifu kwenye safu ya kiungo, Thiago Motta, akiwa mzuri jinsi alivyo lakini sio mchezeshaji mzuri sana kwa mchezo wa kushambulia, hivyo kwenye mechi dhidi ya Ireland, haihatajiki sana. Kwa maana hiyo itabidi Antonio Nocerino aanze kwenye kikosi cha kwanza badala ya Motta. Nocerino ni ni kiungo wa aina ya Box to Box, kiungo ambaye Italy wanahitaji dhidi ya wachezaji aiana ya Keith Andrews na Paul Green, kwa hakika atakuwa mbadla sahihi.

Ikiwa Italy wataendelea mbele kwenye michuano hii itabidi wachezaji wengine waongeze kasi kwenye viwango vyao na kujituma zaidi, na sio kumuachia kiungo mwenye umri wa miaka 33, Pirlo, kubeba mzigo wa taifa kwenye mabega yake.

No comments:

Post a Comment