Mstahiki Meya wa Manispaa ya
Ilala Jerry Silaa akifurahia jambo alipokuwa akimsikiliza Mkurugenzi wa
Montage Bi Teddy Mapunda (kushoto) mara baada ya kuwasili katika eneo
ambapo kulikuwa kunatolewa huduma ya vifaa vya kusaidia usikivu jana
jijini Dar es Salaam. Huduma hii ya kijamii ya kusaidia watu wenye
matatizo ya kusikia imekuwa ikitolewa kwa ushirikiano wa taasisi za
Starkey ya Marekani, Montage ya Tanzania na Serena Hotel ambapo hii ni
mara ya tatu tokea wameanza kutoa huduma hiyo.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya
Ilala Jerry Silaa akimuwekea kifaa cha kusaidia usikivu mwanafunzi
aliyetambulika kwa jina moja la Adrian jana jijini Dar es Salaam.
Mchezaji wa Kimataifa wa Mpira wa Kikapu anayecheza ligi ya NBA nchini Marekani Hasheem Thabeet akiwa na Mwanzilishi wa Starkey ambaye pia ni Daktari bingwa wa magonjwa ya usikivu William Austin alipotembelea kliniki ya kuhudumia wagonjwa wenye matatizo ya usikivu hapa nchini iliyoratibiwa na Taasisi ya kusaidia usikivu (Starkey) kwa kushirikiana na kampuni ya Montage ya Tanzania na Serena Hotel jana jijini Dar es Salaam.
Mchezaji wa Kimataifa wa Mpira wa Kikapu anayecheza ligi ya NBA nchini Marekani Hasheem Thabeet akimpa mazoezi ya kusikia mmoja wa wagonjwa.
Mchezaji wa Kimataifa wa Mpira wa Kikapu anayecheza ligi ya NBA nchini Marekani Hasheem Thabeet akiwa na Mwanzilishi wa Starkey ambaye pia ni Daktari bingwa wa magonjwa ya usikivu William Austin alipotembelea kliniki ya kuhudumia wagonjwa wenye matatizo ya usikivu hapa nchini iliyoratibiwa na Taasisi ya kusaidia usikivu (Starkey) kwa kushirikiana na kampuni ya Montage ya Tanzania na Serena Hotel jana jijini Dar es Salaam.
Mchezaji wa Kimataifa wa Mpira wa Kikapu anayecheza ligi ya NBA nchini Marekani Hasheem Thabeet akimpa mazoezi ya kusikia mmoja wa wagonjwa.
No comments:
Post a Comment